Connect with us

News

Zoezi la kutoa chanjo kung’oa nanga Julai 5

Published

on

Wizara ya Afya imetangaza kampeni ya kutoa Chanjo bila malipo kote nchini katika juhudi za kukabiliana na maradhi ya ukambi, Homa ya tumbo na Surua.

Zoezi hilo la siku 10 linatarajiwa kuanza Julai 5 mwaka huu hadi Julai 14.

Afisa wa masuala ya Chanjo kaunti ya Kilifi Christine Mataza, na mwenzake wa Afya ya Umma Amos Ndenge wamesema zaidi ya watoto elfu 200 walio chini ya umri wa miaka mitano watapokea chanjo ya ukambi na Surua.

Aidha wamesema kwamba zaidi ya Chanjo elfu 200 za Homa ya Matumbo itapeyanwa kwa zaidi ya watoto elfu 600 wa kati ya miezi tisa hadi miaka 14 katika kaunti ya Kilifi.

Chanjo hizo ambazo hutolewa kila baada ya miaka mitano, mwaka huu itaendeshwa katika sehemu za masoko, na shule, kinyume na miaka ya nyuma ambapo zoezi hilo lilikuwa likitekelezwa nyumba hadi nyumba.

Homa ya tumbo husababishwa na matumizi ya maji machafu na Mazingira machafu huku Kenya ikiwa ni Taifa la tano barani Africa kuanzisha Chanjo mpya ya kukabiliana na Huma ya tumbo, ukambi na Surua barani Afrika

Taarifa ya Eric Ponda

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Mahakama kuu yatupilia mbali ombi la Gachagua

Published

on

By

Mahakama kuu imetupilia mbali ombi la pili la aliyekuwa Naibu Rais Rigathi Gachagua la kutaka jopo la majaji watatu wanaosikiliza kesi ya kupinga kubanduliwa wake mamlakani kuzuiliwa kuskiza kesi hiyo. 

Gachagua alisema kwamba majaji hao watatu akiwemo Jaji Eric Ogola, Anthony Mrima na Fridah Mugambi wanafaa kuondolewa kwenye kesi hiyo kwa misingi kwamba uteuzi wao haujazingatia sheria.

Mahakama hiyo ilitupilia mbali ombi hilo, na kusema kwamba jopo hilo la majaji watatu liliteuliwa na Jaji mkuu Martha Koome kwa kuambatana na sheria na kanuni za idara ya Mahakama.

Mahakama imeshikilia kwamba jopo hilo la majaji wa Mahakama kuu litaendelea kusikiliza kesi hiyo hadi wakati wa kutoa uamuzi kwa kuzingatia sheria, na kanuni za idara ya Mahakama pamoja na Katiba ya Kenya.

Mahakama hiyo pia ilitupilia mbali ombi la Mwanaharakati Fredrick Mula ambaye alitaka kubadilishwa kuwa mlalamishi katika kesi nne za kuondolewa mashtaka dhidi ya aliyekuwa Naibu Rais Rigathi Gachagua ambazo alikuwa amewasilisha awali na kisha kutaka kujiondoa.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

News

Wazee wa Kaya wanataka bunge kupitisha sheria kudhibiti mauaji ya wazee

Published

on

By

Muungano wa Wazee wa Kaya kaunti ya Kilifi umeitaka serikali kuu kupitia bunge la kitaifa kubadilisha sheria ya mwaka wa 1926 kuhusu uchawi ili kuwezesha utamaduni kudhibiti mauaji ya wazee yanayoendelea kushuhudiwa kaunti ya Kilifi.

Wakiongozwa na Stanley Kahindi Kiraga wamesema kuwa sheria hiyo imechangia pakubwa mauaji ya wakongwe Kilifi kutokana na swala kuwa haitambui uwepo wa uchawi na jinsi ya kuudhibiti.

Kiraga sasa anasema ni sharti sheria hiyo iondolewe au ifanyiwe ukarabati bungeni hali itayopelekea uchawi kudhibitiwa kupitia mila na utamaduni.

“Vijana wanaowaua wazee wakiwasingizia kuwa wachawi wanazidi kuongezeka na kwa sababu hakuna sheria ya moja kwa moja ya kuwashtaki na kuwafunga” amesema Kiraga akieleza kusikitishwa kwake na ongezeko la magenge ya vijana wanaolipwa kutekelezwa mauaji ya wazee kwa shutuma za uchawi.

Taarifa ya Hamis Kombe

Continue Reading

Trending