News

Watu watatu wakamatwa katika Mahakama ya Milimani

Published

on

Watu watatu wanaodaiwa kuwa wafanyakazi wa kaunti ya Trans Nzoia wamekamatwa na maafisa wa polisi waliokuwa wamevalia sare baada ya kusikiza kesi inayomkabili gavana wa kaunti hiyo George Natembeya katika Mahakama ya Milimani jijini Nairobi.

Watatu hao walikamtwa mda mfupi baada ya Jaji Zipporah Gichana, kuagiza upande wa mashtaka kuwasilisha ushahidi dhidi ya kesi ya ufisadi inayomkabili gavana huyo.

Agizo hilo lilifuata tamko la upande wa mashtaka kwamba ilifeli kufuta agizo la awali la Mahakama la kuwasilisha ushahidi.

“Nyaraka na taarifa hizo zilipaswa kuwa zimetolewa kufikia sasa, kwa hiyo ninaelekeza upande wa mashtaka kufuata maagizo ya awali”, aliagiza Jaji Gichana.

Upande wa mashtaka uliomba mda wa wiki mbili zaidi ili kutii maagizo ya awali ya kuwasilisha ushahidi wa nyaraka.

“Hati nyingi zinapatikana kutoka kaunti ya Trans Nzoia na tumeshindwa kuzipata, tunaomba wiki mbili za ziada ili kutii,” Wakili wa Serikali Victor Awiti aliwasilisha.

Hata hivyo, upande wa utetezi ulipinga ombi hilo, ukisema ni sawa na matumizi mabaya ya mchakato wa Mahakama.

Upande wa mashtaka uliamriwa kufichua nyenzo zote husika kabla ya Juni 16 kesi hiyo itakapotajwa.

Taarifa ya Joseph Jira

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version