News

Wanaharakati wa Kutetea Haki za Kibinadamu Waandamana Mombasa

Published

on

Wanaharakati wa kutetea haki za kibinadamu kaunti ya Mombasa wamefanya maandamano hadi katika ofisi za ubalozi wa Tanzania mjini Mombasa wakitaka kuachiliwa huru kwa Mwanaharakati wanaozuliwa nchini Tanzania.

Wakiongozwa na Mkurugenzi wa Shirika la Haki Afrika Wakili Yusuf Abubakar, Wanaharakati hao wamesisitiza umuhimu wa haki za kibinadamu kulindwa huku wakiitaka serikali ya Tanzania kuheshimu haki za Wanaharakati hao.

Wakili Abubakar amesisitiza kuachiliwa kwa Wanaharakati hao huku akilaani vikali kuzuiliwa kwao, akisema Wanaharakati hao walizuru taifa hilo kufuatilia kesi ya Kiongozi wa upinzani nchini humo Tundu Lisu.

Kwa upande wake Afisa wa masuala ya dharura katika Shirika la kutetea haki za kibinadamu la MUHURI Francis Auma ametaka Wanaharakati Boniface Mwangi na Agather Haire ambao bado wanazuliwa nchini humo waachiliwe mara moja.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version