News

Wakaazi wa Magarini wanalalamikia uhaba wa maji

Published

on

Wakaazi wa Magarini kaunti ya Kilifi wanalalamikia kukithiri kwa changamoto ya uhaba wa maji inayoendelea kushughudiwa katika eneo hilo.

Wakiongozwa na Joseph Kithi, wakaazi hao walielezea kusikitishwa na jinsi eneo hilo limesalia bila huduma za maji kwa kipindi kirefu.

Aidha walisema maeneo mengine ya kaunti ya Kilifi yakipata maji kwa urahisi, itakuwa jambo mwafaka katika kufanikisha miradi mbalimbali ya kimaendeleo lakini suala hilo limekosa kuangizwa na kuchangia wanawake wengi kupitia changamoto.

Kithi alidokeza kwamba kwa sasa eneo hilo limebaki bila huduma za maji kwa takriban miezi miwili, akiilaumu serikali kwa kutoangazia mikakati ya kusuluhisha changamoto hiyo.

“Sisi wakaazi wa Magarini tumekuwa tukipita changamoto nyingi sana za ukosefu wa maji, jambo la kusitisha ni kwamba maji yanatoka hapa karibu na maeneo yetu LangoBaya lakini ichukua mda mrefu bila maji, kwani haya maji yanaenda wapi kwani shinda ya maji imekuwa miaka nenda miaka rudi inachukua mda mrefu bila maji”, alisema Kithi.

Wakaazi hao waliiomba serikali kuhakikisha kwamba huduma za maji zinarudishwa haraka iwezekanavyo la sivyo wataandamana hadi pale changamoto hiyo itakapoangaziwa kikamilifu na wananchi kupata maji.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version