News
Waislam Waadhimisha Sikukuu ya Eid-Ul-Adha
Waislam kote duniani wanaadhimisha Sikukuu ya Eid-Ul-Adha, inayojulikana pia kama sikukuu ya sadaka, ambayo huadhimishwa katika mwezi wa Dhul Hijjah katika kalenda ya Kiislam.
Sikukuu hii ni moja ya nyakati tukufu zaidi katika Uislamu, ikiashiria kilele cha Hijja na kuadhimisha utiifu wa Nabii Ibrahimu aliyekuwa tayari kumtoa mwanawe Ismail kama sadaka kwa amri ya Mwenyezi Mungu.
Siku kumi za mwanzo za Dhul Hijjah zinahesabiwa kuwa siku takatifu zaidi, zikiwa zimejawa na ibada, kufunga, na dua.
Mwaka huu, zaidi ya mahujaji milioni 2 wanahudhuria Hijja katika mji mtakatifu wa Makkah nchini Saudi Arabia, Kenya ikipeleka wahujaji 4,500, kuhijji, ikiwa ni mojawapo ya idadi kubwa zaidi katika historia ya hivi karibuni.
Viongozi mbalimbali wa dini ya kiislam waliwahimiza waumini wa dini ya kiislam kuhakikisha wanasheherekea sikukuu ya Eid-ul-Adha pamoja na wale wasiojiweza kwa kuchinja mifugo na kugawa na watu wengine wasiobahati katika jamii.
Taarifa ya Lolani Kalu