Sports
Harambee Stars Kuvaana Na Chad Mechi Ya Kirafiki.
Timu ya Taifa Harambee Stars chini ya kocha Benni Mccarthy kushuka dimbani majira saa kumi jioni Ugani Stade de Marrakech Morocco ikiwa ni mechi ya kirafiki.
Kwa mujibu wa mwalimu wa Stars Mccarthy mechi hizi ni muhimu kujenga kikosi kwa majukumu ya siku za usoni lakini pia kwa taji la Chan sawa na Afcon mwaka 2027.
“Ni muda mzuri mimi kufahamu vijana wangu na kuanza kuanda timu yenye ubora kwa minajili ya siku za usoni na wachezaji wa nyumabani watasaidia sana CHAN mwezi Agosti.”
Baada ya mechi hiyo Stars watacheza mechi nyingine na taifa hilo Juni 10.
Rais wa Fkf Hussein Mohammed amekariri kikosi hicho kitaelekea Uarabuni kwa maozezi kabambe kabila ya Chan humu nchini.