News

Chengo, awahimiza viongozi wa Pwani kutumia nafasi zao vizuri

Published

on

Mwakilishi wa wadi ya Tezo kaunti ya Kilifi, Thomas Chengo alitoa wito kwa viongozi wa Pwani kutumia nafasi walizo nazo katika uongozi wa Kenya Kwanza ili kuboresha kaunti za Pwani kimaendeleo.

Chengo ambaye pia ni Kiongozi wa walio wachache katika bunge la kaunti ya Kilifi, alisema kuna viongozi wengi wa Pwani ambao wako serikalini na ikiwa watatumia fursa hiyo ipasavyo huenda wapwani wakanufaika zaidi kupitia miradi mbalimbali.

Kulingana na Chengo, hii ndio mara ya kwanza kwa wapwani kuwa na viongozi wengi serikalini na akasisitiza umuhimu wa ushirikiano ili kuliboresha eneo la Pwani kama maeneo mengine nchini.

“Nataka ijulikane kwamba hii sio ajali na ikiwa hatutashikana vizuri, tukatumia hii nafasi vizuri nafasi hii kujirudia tena sio rahisi’’, alisema Chengo.

Vilevile aliwashinikiza viongozi wa kaunti ya Kilifi kuwahudumia wenyeji na kutekeleza miradi ya maendeleo badala ya kunyoshea kidole cha lawama kwa masuala ambayo hayana manufaa.

Taarifa ya Janet Mumbi

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version