Sports

Tottenham Yamfuta Kazi Kocha Postecoglou

Published

on

Kilabu ya Tottenham Hotspurs ya London Kaskazini imetangaza kumfuta kazi kocha wake Ange Poetecoglou siku cheche tu baada ya mwalimu huyo kuongoza kilabu yake kuvunja ukimya wa miaka 17 na kutua taji la UEFA Europa Ligi kwa kushinda Manchester United goli 1-0 ugani San Mames Uhispania Mei 21.

Kwenye taarifa kwa vyombo vya habari kilabu hiyo kupitia kwa mwenyekiti wake Daniel Levy imesema kwamba imeweza kupiga msasa utenda kazi wa kocha huyo katika msimu mzima na hivyo basi kukubaliana kumuonyesha mlango raia huyo wa Australia.

Spurs walimaliza nafasi ya 17 jedwali la Ligi ya Uingereza na alama 38 na matokeo hayo huenda yamechangia kufurusha kwa mwalimu huyo kocha huyo akipoteza mechi 21.

Postecoglou si wa kwanza kufutwa kazi na spurs katika njia tatanishi wengine ni kocha Jose Mourinho,Nuno Espirito Dos Santos na Mauricio Pochettino.

Hata hivyo taarifa hiyo haijachukulia vyema na baadhi ya wachezaji ambao wameshutuliwa na taarifa hiyo baada ya ufanisi wa kocha huyo Spurs.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version