Connect with us

Sports

Tottenham Yamfuta Kazi Kocha Postecoglou

Published

on

Kilabu ya Tottenham Hotspurs ya London Kaskazini imetangaza kumfuta kazi kocha wake Ange Poetecoglou siku cheche tu baada ya mwalimu huyo kuongoza kilabu yake kuvunja ukimya wa miaka 17 na kutua taji la UEFA Europa Ligi kwa kushinda Manchester United goli 1-0 ugani San Mames Uhispania Mei 21.

Kwenye taarifa kwa vyombo vya habari kilabu hiyo kupitia kwa mwenyekiti wake Daniel Levy imesema kwamba imeweza kupiga msasa utenda kazi wa kocha huyo katika msimu mzima na hivyo basi kukubaliana kumuonyesha mlango raia huyo wa Australia.

Spurs walimaliza nafasi ya 17 jedwali la Ligi ya Uingereza na alama 38 na matokeo hayo huenda yamechangia kufurusha kwa mwalimu huyo kocha huyo akipoteza mechi 21.

Postecoglou si wa kwanza kufutwa kazi na spurs katika njia tatanishi wengine ni kocha Jose Mourinho,Nuno Espirito Dos Santos na Mauricio Pochettino.

Hata hivyo taarifa hiyo haijachukulia vyema na baadhi ya wachezaji ambao wameshutuliwa na taarifa hiyo baada ya ufanisi wa kocha huyo Spurs.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Manchester United Ndiyo mabingwa wa ‘PREMIERE LEAGUE SUMMER SERIES’

Published

on

By

Manchester United imetwaa ubingwa wa kombe la ‘Premier League Summer Series’ kufuatia sare ya 2-2 dhidi ya Everton katika dimba la Mercedes-Benz, Atlanta, Georgia Marekani.
Michuano hiyo ya maandalizi ya msimu mpya ilishirikisha timu nne za Ligi Kuu England Man United, West Ham United, Everton na Bournemouth ambapo Mashetani hao Wekundu wamemaliza kileleni pointi 7 baada ya mechi tatu, wakishinda mechi mbili na kutoka sare mechi moja.
Kiungo Bruno Fernandes aliwaweka uongozini United dakika ya 18 kupitia mkwaju wa Penalti au Tuta kisha Iliman Ndiaye akisawazishia The Toffees dakika ya 40,United tena walichukua uongozi kupitia kwa kiungo mshambulizi Mason Mount dakika ya 69 kabila ya beki Ayden Heaven kujifunga dakika ya 75.
MSIMAMO:
1. Man UTD — mechi 3 — pointi 7
2. West Ham mechi 3 — pointi 6
3. Bournemouth mechi 3 — pointi 3
4. Everton mechi 3 — pointi 1
Continue Reading

Sports

Stars yaanza vema CHAN kwa ushindi goli 1-0 dhidi ya DR-Congo

Published

on

By

Timu ya Taifa ya Kenya (Harambee Stars) imechukua alama zote tatu kufuatia ushindi wa 1-0 dhidi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kwenye mchezo wa kwanza wa Kundi B wa kombe la Mataifa Afrika CHAN 2024 katika dimba la Moi Sports Centre, Nairobi.
Goli hilo la kipekee lilitiwa wavuni na kiungo mshambulizi Austine Odhiambo dakika 45 kipindi cha kwanza.
Rais William Ruto ambaye alifuatilia mechi hiyo uwanjani alitembelea kikosi katika chumba cha kubadilisha na kukabidhi ahadi yake ya shilindi milioni moja kwa kila mchezaji baada ya ushindi huo.
Stars wamekwea kileleni mwa kundi A na alama Tatu kundi ambalo pia lina Morocco,Zambia na Angola Mechi ijayo ya Stars ni dhidi ya Angola ni Agosti 7.
Continue Reading

Trending