Sports
Tottenham Yamfuta Kazi Kocha Postecoglou

Kilabu ya Tottenham Hotspurs ya London Kaskazini imetangaza kumfuta kazi kocha wake Ange Poetecoglou siku cheche tu baada ya mwalimu huyo kuongoza kilabu yake kuvunja ukimya wa miaka 17 na kutua taji la UEFA Europa Ligi kwa kushinda Manchester United goli 1-0 ugani San Mames Uhispania Mei 21.
Kwenye taarifa kwa vyombo vya habari kilabu hiyo kupitia kwa mwenyekiti wake Daniel Levy imesema kwamba imeweza kupiga msasa utenda kazi wa kocha huyo katika msimu mzima na hivyo basi kukubaliana kumuonyesha mlango raia huyo wa Australia.
Spurs walimaliza nafasi ya 17 jedwali la Ligi ya Uingereza na alama 38 na matokeo hayo huenda yamechangia kufurusha kwa mwalimu huyo kocha huyo akipoteza mechi 21.
Postecoglou si wa kwanza kufutwa kazi na spurs katika njia tatanishi wengine ni kocha Jose Mourinho,Nuno Espirito Dos Santos na Mauricio Pochettino.
Hata hivyo taarifa hiyo haijachukulia vyema na baadhi ya wachezaji ambao wameshutuliwa na taarifa hiyo baada ya ufanisi wa kocha huyo Spurs.
Sports
Harambee Stars Kuvaana Na Chad Mechi Ya Kirafiki.

Timu ya Taifa Harambee Stars chini ya kocha Benni Mccarthy kushuka dimbani majira saa kumi jioni Ugani Stade de Marrakech Morocco ikiwa ni mechi ya kirafiki.
Kwa mujibu wa mwalimu wa Stars Mccarthy mechi hizi ni muhimu kujenga kikosi kwa majukumu ya siku za usoni lakini pia kwa taji la Chan sawa na Afcon mwaka 2027.
“Ni muda mzuri mimi kufahamu vijana wangu na kuanza kuanda timu yenye ubora kwa minajili ya siku za usoni na wachezaji wa nyumabani watasaidia sana CHAN mwezi Agosti.”
Baada ya mechi hiyo Stars watacheza mechi nyingine na taifa hilo Juni 10.
Rais wa Fkf Hussein Mohammed amekariri kikosi hicho kitaelekea Uarabuni kwa maozezi kabambe kabila ya Chan humu nchini.
Sports
Kenya Pipeline Yaanza Kwa Kishindo Fainali Ya Voliboli

Kilabu ya Kenya Pipeline ilianza kwa kishindo fainali ya taji la akina dada mchezo wa voliboli mashidano yanayondelea uwanjani Kasarani Indoor Arena jijini Nairobi.
Hii ni baada ya vipusa hao chini ya kocha Godfrey Omondi kuwatandika wenzao DCI seti 3-0 mechi ya ufunguzi uwanja huo ukifurika hadi pomoni.
Kikosi hicho kilishinda mechi hiyo kwa seti 25-19,25-20,25-14 na kuibuka na ushindi huo mnono kabila ya mechi ya pili jumamosi.
Nahodha wa KPC Gladys Ereng amesema kwamba mechi haikua rahisi kwani DCI walikua vizuri ila walipambana kwa ushindi huo.
“DCI ni timu nzuri walicheza vizuri kipindi cha kwanza kwani tulianza kwa utepetevu ila tukazungumza na kujikusanya vyema na kupata ushindi huo muhimu kwetu.”
Kwa Upende wake kocha wa DCI Patrick Sang amedokeza kwamba hakucheza kwa umakinifu waliotarajia;”Hatukucheza kwa mipangilio yetu mazungumzo pamoja na utulivu haikuwepo lakini ndio hali ya mchezo nipongeze wenzetu.”
Kilabu ya General Service Unit (GSU) upande wa wanaume ilianza vema kusaka taji la upande wa Wanaume baada ya kushinda mechi ya mkondo kwanza sati 3-0 katika uwanja huo huo.
Hii ni baada ya kuwatandika Kenya Ports Authority (KPA) seti 3-0 za 25-15,25-22,30-28