Sports

Stars Kambini Kwa Maandalizi Ya CHAN

Published

on

Timu ya Taifa ya soka Harambee Stars kimeingia kambini tayari kwa maandalizi ya Chan mwezi ujao katika mataifa ya Kenya,Uganda na Tanzania.

Vijana wa Nyumbani wamekaribishwa kambini na Waziri wa michezo Salim Mvurya na katibu mkuu Elija Mwangi na,rais wa Shirikisho la soka FKF Hussein Mohammed.

Stars itaendeleza mazoezi ugani Ulinzi Sports Complex chini ya kocha mkuu Benni MacCarthy ambaye amesema kwamba wako katika hali shwari,alipoulizwa kuhusu wachezaji wengine kukosana kikosini mwalimu huyo amedai kwamba hawezi akafurahisha kila mmoja wakati wa Uteuzi.

“Huwezi kumpendeza kila mtu,Sijakuja kufurahisha kila mtu ila malengo yake ni kuteua kikosi bora kwa ajili ya Taifa,Ni mimi ndiye kocha na nimetazama hawa wachezaji kwa hivyo lengo ni kunoa stars kuleta matokeo chanya timuni.”

Stars watakua kambini kabila ya kuelekea Tanzania kwa taji la CECAFA mataifa manne ;Kenya, Uganda,Tanzania na Sudan Kusini.

 

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version