News

Shule Ya Upili Ya Serani Ndiyo Mabingwa Eneo La Mvita

Published

on

Timu ya shule ya upili ya Serani imetetea ubingwa wao wa eneo la Mvita baada ya kuwalaza Tononoka magoli 2-1 katika fainali iliyochezewa kwenye uwanja wa shule ya upili ya Khamis.

Emanuel Oroni aliwatanguliza Serani na goli la kwanza kupitia mkwaju wa penati kabla ya Ali Abdallah kusawazishia Tononoka, lakini goli lake Emanuel Ngala katika kipindi cha pili likawapa ubingwa huo.

Kulingana na kocha wa Serani Alex Shikanga ni kwamba wamekua na mazoezi kambambe kabila ya mashindano ya shule za Upili na walikua wanasubiri ushindi tu wala si kitu kingine.

“Tulikua tumejiandaa kwa ajili ya ushindi pekee tumekua na maandalizi mazuri na hivyo nilijua tuatshinda fainali hii,katika miaka mitano tumepoteza taji hili mara moja pekee.”

kwa upande wake kocha wa Shule ya Upili ya Tononoka Juma ALi Kalato amesema kwamba amesema kwamba amekubali matokeo baada ya changamoto si haba kabila ya mechi hiyo ya fainali baadhi ya wachezaji wakingonjeka.

“Nashukuru Mwenyemezi Mungu tumefika fainali na vijana wangu wamepambana kiume kwani kabila ya mechi tulikua na wagonjwa ila wamepambana inshallah tutashinda uko mbele.”

Katika upande wa wasichana Kaa Chonjo wameibuka mabingwa kwa kuwalaza Mekatitilili magoli 3-0.

Serani na  Tononoka wataiwakilisha Mvita katika ngazi ya kaunti upande wa wavulana, na Kaa Chonjo na Mekatililii wakiwakilishja upande wa wasichana.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version