News
Rais Ruto atia saini Miswada miwili kupiga jeki Mgao wa Serikali za Kaunti
Rais William Ruto ametia saini na kuwa sheria miswaada miwili muhimu inayokusudiwa kupiga jeki ufadhili wa Serikali za Ugatuzi nchini.
Rais Ruto ambaye anahudhuria Kongamano la Ugatuzi mwaka huu katika kaunti ya Homa Bay, ametia saini mswada kuhusu Ugavi wa pato la serikali kwa hazina za Kaunti wa 2025, na pia Mswada mwengine unaotoa muongozo wa matumizi ya fedha za serikali za Kaunti wa 2023.
Mswaada unaohusu usimamizi na muongozo wa matumizi ya pesa za kaunti sasa umefutiliwa mbali na kubuni Hazina ya mabunge ya Kaunti zote 47.
Mswaada huo wa nyongeza ya pato kwa kaunti umeongoza kiwango cha hapo awali kutoka Shilingi billioni 387.4 mwaka uliopita hadi kiwango cha Shilingi bilioni 415 katika kipindi cha mwaka huu 2025/26 cha matumizi ya pesa serikalini.
Hafla hiyo ya kutia saini miswaada hiyo miwili,imefanyika katika Ikulu ndogo kaunti ya Homabay Jumatano Agostu 13 2025.
Mswaada huo uliowasilishwa bungeni na Senta wa Meru Kathuri Murungi, unayapa uhuru zaidi Mabunge ya Kaunti katika masuala ya usimamizi wa fedha zao.
Hatua hiyo imetokea wakati Kongamano la Ugatuzi limefunguliwa rasmi katika Kaunti ya Homabay, kutathmini mafanikio na changamoto kwa serikali za Kaunti.
Kongamano hilo linahudhuriwa miongoni mwa wengine Wafanyi biashara na washika Dau mbali mbali wa kimaendeleo katika ngazi za Kaunti.
Hazina kuu ya Serikali sasa inatarajiwa kuhakikisha kuwa mgao huo wa fedha unafikia hazina za serikali za Kuanti kabla ya tarehe 15 ya kila mwezi
Katika muda wa miaka miwili iliyopita serikali kuu ya kitaifa imeshtumiwa vikali na Baraza la Magavana, kwa madai ya njama za kuhujumu Ugatuzi nchini.
Taarifa ya Eric Ponda