Business
Mvua Yawaathiri Wafanyikazi wa Fuo za Bahari Mombasa
Wafanyikazi wa fuo za bahari katika Kaunti ya Mombasa wamelalamikia athari za mvua zinazoendelea kunyesha, wakisema hali hiyo imepunguza shughuli zao za kila siku na kuathiri mapato yao.
Wakizungumza na vyombo vya habari, wafanyikazi hao wamesema kuwa mvua kubwa iliyoshuhudiwa katika kipindi hiki imechangia kupungua kwa idadi ya watalii wanaotembelea fuo hizo, hali ambayo imesababisha kupungua kwa kipato chao.
Aidha, wamesema kuwa bahari kwa sasa inakumbwa na mawimbi makali na mazingira hatarishi, jambo linalowaogopesha watalii na kuwazuia kufika kwenye maeneo ya ufukweni.
Hata hivyo, wameeleza kuwa wana matumaini kuwa hali hiyo ni ya muda na biashara zao zitaimarika pindi hali ya hewa itakaporejea kuwa ya kawaida.