News
Mpango wa Usambazaji Maji Kilifi Kuendelea
Serikali ya kaunti ya Kilifi kwa ushirikiano na serikali ya kitaifa kupitia Shirika la usambazaji umeme la REREC wanaendeleza mpango wa usambazaji umeme katika kaunti ya Kilifi.
Gavana wa kaunti hiyo, Gedion Mung’aro, amesema mpango huo unalenga kufikisha huduma za umeme mashinani ili kufanikisha shughuli mbalimbali za kibiashara kwa urahisi.
Gavana Mung’aro amedokeza kwamba Shirika la REREC na kaunti ya Kilifi wamekuwa wakiwekeza kiwango flani cha fedha katika mpango huo ili kuhakikisha wakaazi wanapata huduma za umeme hadi mashinani.
Wakati huo huo amebainisha kwamba serikali ya kaunti ya Kilifi inaendeleza mradi wa usambazaji maji katika eneo bunge la Magarini katika juhudi za kukabiliana na changamoto ya uhaba wa maji eneo hilo.