Sports
Liverpool Kuwasilisha Ofa Mpya Kusajili Wirtz
Mabingwa wapya wa ligi ya Epl liverpool inatarajiwa kuwasilisha ofa nyingine kusaka hudumza kiungo matata wa Ujerumani Florian Wirtz.
Hii ni Baada ya kilabu ya Bayer Leverkusen kukataa ofa ya pauni milioni 113 kutoka kwa usajli wa mchezaji huyo ambaye ameweka wazi yuko tayari kujiunga na The Reds msimu ujao.
Leverkusen imeshikilia kuwa inahitaji kitita cha pauni milioni 126 kumwachilia nyota huyo mwenye umri wa miaka 22 ambaye pia anamezewa mate na Real Madrid ya Uhispania na Manchester City wa Uingereza.
Inaaminika mchezaji huyo ndiye atakua sajili wa kwanza kwa kocha mkuu Arne Slot msimu huu wakiwa tayari kuwachiliwa nyota wake akiwemo mshmabulizi Darwin Nunez,Federico Chiesa,Harvey Elliot na Kostas Tsimiskas ambao wote wataondoka ugani Anfield.