News
Mpango wa Usambazaji Maji Kilifi Kuendelea

Serikali ya kaunti ya Kilifi kwa ushirikiano na serikali ya kitaifa kupitia Shirika la usambazaji umeme la REREC wanaendeleza mpango wa usambazaji umeme katika kaunti ya Kilifi.
Gavana wa kaunti hiyo, Gedion Mung’aro, amesema mpango huo unalenga kufikisha huduma za umeme mashinani ili kufanikisha shughuli mbalimbali za kibiashara kwa urahisi.
Gavana Mung’aro amedokeza kwamba Shirika la REREC na kaunti ya Kilifi wamekuwa wakiwekeza kiwango flani cha fedha katika mpango huo ili kuhakikisha wakaazi wanapata huduma za umeme hadi mashinani.
Wakati huo huo amebainisha kwamba serikali ya kaunti ya Kilifi inaendeleza mradi wa usambazaji maji katika eneo bunge la Magarini katika juhudi za kukabiliana na changamoto ya uhaba wa maji eneo hilo.
News
Kalonzo, Gachagua Wapinga Ujenzi wa Kinu cha Nuklia Kilifi

Viongozi wa Upinzani wakiongozwa na kinara wa chama cha Wiper, Kalonzo Musyoka, wamepaza sauti kupinga ujenzi wa kinu cha Nuklia katika eneo la Uyombo wadi ya Matsangoni Kaunti ya Kilifi.
Wakihutubu mjini Malindi Kaunti ya Kilifi viongozi hao akiwemo kinara wa DCP, aliyekuwa Naibu wa Rais Righathi Gachagua na mwenzake wa DAP, Eugene Wamalwa, waliongeza kwamba tayari wamewaagiza mawakili kuwasilisha kesi mahakamani kupinga mradi huo.
Waliyasema haya baada ya kuhudhuria misa ya Jumalipili katika katika Kanisa la JCC iliyoongozwa na Askofu Kakala mjini humo katika siku ya pili ya ziara yao ya ukanda wa Pwani.
Kalonzo alizidisha makombora yake Kwa serikali ya Rais William Ruto akiitaka iwajibikie maovu yake ya visa vya utekaji nyara na mauaji ya Vijana wa kizazi cha Gen-Z wakati wa Maandamano mwaka uliopita.
Kiongozi huyo alisema kwamba mnamo tarehe 25 mwezi huu wa Juni 2025, upinzani utawaongoza wakenya kuwakumbuka vijana waliouawa wakati wa Maandamano hayo ya Gen-Zs mwaka uliopita, kwa kuwasha mishumaa nje ya majengo ya bunge.
Kiongozi wa DCP, na aliyekuwa Naibu wa Rais Righathi Gachagua alisema serikali ya Kenya Kwanza, inaendelea kupora pesa za wafanyi kazi kutoka hazina ya malipoa ya Uzeeni NSSF, na kuzitumia Kwa miradi ya kibinafsi katika eneo la Bomas.

Picha kwa hisani
Kwa upande wake Kiongozi wa DAP, Eugene Wamalwa alisema kwamba serikali ya Rais Ruto sasa inatumia pesa za ushuru wa nyumba kujenga masoko katika Kaunti mbali mbali kama njia Moja wapo ya mbinu za kuwashawawishi viongozi hasa Magavana,kuunga mkono serikali ya KK, na kuongeza Kwamba ujenzi wa masoko ni jukumu la serikali za ugatuzi.
Viongozi hao waliwahutubia wananchi katika soko la Kwajiwa mjini Malindi, huku msafara huo ukisimama eneo la Matsangoni, Chuo kikuu Cha Pwani mjini Kilifi, na mji wa Mtwapa.
Taarifa ya Eric ponda
News
Chama cha DCP chashinikiza wakenya kupinga mswada wa fedha, 2025

Uongozi wa chama cha DCP unashinikiza wakenya kupinga mswada wa fedha wa mwaka 2025 ukidai una vipengee tata vitakavyoongeza mzigo wa ushuru kwa wakenya.
Kulingana na Naibu Kinara wa chama hicho Cleophas Malala, mswada huo hauzingatii hali ya uchumi ya wakenya ambao wanaendelea kukabiliana na gharama ya juu ya maisha.
Malala alitaja baadhi ya vipengee vinavyoibua maswali kama vile kodi mpya ya kuongezwa kwa ushuru wa VAT kwenye bidhaa za kawaida kama vile vyakula.
Akizungumza mjini Mombasa, Malala alishauri wakenya kuwa makini na kushiriki mchakato wa kuchambua mswada huo kikamilifu vile vile kutoa maoni kwa bunge kabla ya kupitishwa na kuwa sheria.
Malala alimlaumu Kinara wa chama cha ODM Raila Odinga pamoja na Rais William Ruto akidai wamezihadaa familia zilizowapoteza wapendwa wao mwaka jana wakati wa maandamano ya kupinga mswada wa fedha kwamba zingefidiwa.
Taarifa ya Joseph Jira.