Sports

Kenya Pipeline Ndiyo Mabingwa Voliboli Akina Dada

Published

on

Kilabu ya Kenya Pipeline ndiyo mabingwa wa taji la akina dada ligi ya Voliboli baada ya kushinda kilabu ya DCI seti 3-2 (21-25, 25-21, 18-25, 25-21, 15-11) fainali kali iliopigwa ugani Kasarani Indoor Arena wikendi.

Kulingana na Kocha mkuu George Omondi amefurahishwa na matokeo hayo licha ya upinzani kuwa mkali zaidi,

“Tulihitaji Kucheza vizuri mpaka mwisho,Tulijua ni lazima tucheze kwa ukakamavu mkubwa kwani si mechi rahisi katika fainali ila wasichana wangu wamekakamua kufanya kweli na kuvuna ushindi huu ambao ni wa kipekee.”

Kocha wa DCI Patrick Sang aliweza kushukuru wapinzani wake kwa kushinda hata hivyo akishikilia kufika katika fainali si jambo jepesi tangu wajaribu kwanzia mwaka 2018.

“Nimeridhika na Matokeo wasichana hao wamecheza kwa ushujaa mkubwa tulitaka taji ila nimeridhika na nafasi ya pili kuwa nafasi ya pili si mabya kwetu ni matokeo bora zaidi.”

Upande wa wanaume kinyanganyiro ni kati ya GSU na KPA.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version