News

Miili 7 zaidi yagunduliwa Kwa Binzaro na kufikisha idadi ya miili 32

Published

on

Shughuli ya kufukuaji wa maiti katika vichaka vya Kwa Binzaro eneo la Shakahola kaunti ndogo ya Magarini inaingia wiki ya pili huku miili 7 zaidi ikifukuliwa Alhamisi Agosti 28.

Kupatikana kwa miili hiyo sasa inafikisha idadi ya maiti zilizofukuliwa katika kijiji Kwa Binzaro kuwa watu 32 waliofariki katika awamu ya pili ya sakata ya mauaji ya kinyama eneo la Shakahola.

Maafisa wa serikali wa uchunguzi wa maiti wakiongozwa na Daktari Richard Njoroge, walisema miili hiyo iliharibika kiasi cha kutombulika huku wakipata vipande vingine 54 vya miili vikiwa vikitapakaa katika eneo la tukio.

Hii inaaminika kwamba baadhi ya miili hiyo ililiwa na wanyamapori kwani ilikuwa imezikwa katika makaburi ya kina kifupi sana.

Sakata hii ya Shakahola 2 inazidisha hofu hasa miongoni mwa wakaazi wa sehemu hiyo ya Shakahola kukiwa na taarifa kwamba huenda baadhi ya miili hiyo ilisafirisha hadi eneo hilo la Kwa Binzaro.

Mapema mwezi uliopita maafisa wa usalama, kwa ushirikiano na wenyeji walifumania kundi la watu wanaoaminika kwamba ni wafuasi wa itikadi kali katika msitu huo wa Kwa Binzaro ambao baadhi yao walifanikiwa kutoroka.

Maafisa wa Polisi waliwazuilia korokoroni watu sita kuhusiana na sakata hiyo ya Kwa Binzaro, ambayo imetokea miaka michache tu tangu kisa cha kwanza na shakaola One chini ya uongozi wa Mhubiri tata Paul Mackenzie.

Waumini wa Kanisa la Mhubiri Mackenzie waaminika walilazimishwa kufunga hadi kufa kwa imani kwamba watakutana na Yesu.

Mackenzi na wenzake wako korokoroni wakisubiri uamuzi wa Mahakama kuhsu kesi ya mauaji inayowakanili.

Taarifa ya Eric Ponda

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version