News

Mchawi anaswa na wenyeji, Mavueni

Published

on

Kulikuwa na kizaazaa Julai mosi 2025 katika kijiji cha Mabirikani eneo la Eureka Mitangoni karibu na Mavueni kaunti ya Kilifi baada ya mwanamume anayedaiwa katumia nguvu za uchawi kupatikana ndani ya nyumba, kitandani.

Mwanamme huyo alipatikana akiwa amevalia shati na kikoi cha mwenye nyumba ambaye anaishi jijini Mombasa na mkewe.

Ilisemekana wawili hao hakuweko ndani ya nyumba yako wakati wa tukio hilo lililowashangaza wengi.

Umati wa watu uliwasili katika jumba hilo la ghorofa wakiwa na ghadhabu wakitaka kumshambulia mshukiwa anayedaiwa kuwa mchawi.

Maafisa wa polisi walidumisha usalama wakati walipokuwa wakimsubiri mwenye nyumba kuwasili eneo la tukio kutoka jijini Mombasa.

Alipowasili Japhet Mumba, mwenye nyumba iliyonaswa mshukiwa wa mchawi, alithibitishia umati kuwa mshukiwa alikuwa ndani yanyumba yake na alikuwa amevalia baadhi ya nguo zake.

Kulingana na mtoto wa mzee mwenye nyumba, mtuhumiwa kwa jina Samson ambaye alikuwa na kitambaa chekundu mkononi, inadaiwa alipenya nyumbani akiwa uchi na akashindwa kutembea.

Aliongeza kuwa alipofika mlangoni alisimama hapo hadi mwenye nyumba alipofika na kumhoji.

Ilibainika nguo za mshukiwa alizozivua zilikuwa zingali nje ya nyumba alimokamatwa.

” Mimi niliona hii nyumba ina matatizo makubwa. Nisameheni”, alisema mshukiwa huyo wa ushirikina.

Ililazimu polisi waondoke na mtuhumiwa huyo ili kumnusuru kutoka kwa umati uliojawa na hasira.

Taarifa ya Lolani Kalu

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version