News
Mauaji ya wazee kwa shutma za uchawi yapungua Rabai-Kilifi.
Idara ya usalama kaunti ya Kilifi imetaja kupungua kwa visa vya mauaji ya wazee wanaohusishwa na tuhma za uchawi katika eneo bunge la Rabai.
Naibu Kamishna wa eneo hilo Joseph Lenkarie alikiri kuwa visa hivyo vilikuwa vimekithiri eneo hilo huku akiwahimiza wakaazi kuendelea kuzingatia usalama wa wazee.
Wakati huo huo aliwataka maafisa wa utawala wa mkoa eneo hilo kuhakikisha mradi wa usambazaji umeme mashinani unatekelezwa ili kuwafaidi wananchi.
“Yale maneno tulikuwa tunapiga wazee ni ukweli tumeacha, sini ukweli ama bado mnapiga wazee? ya pili nimeambiwa tuliletewa umeme, wale machifu miradi ya stima inafanyika kwenu, lazima mjue yale mambo watu wa Kenya Power walisema na ni lazima tujuwe kama wamefanya hiyo kazi hatutaki kudanganya wananchi”, alisema Lenkarie.
Alisema ni jukumu la machifu kuhakikisha wanafuatilia kwa karibu miradi yote iliyoanzishwa na serikali ili kuhakikisha inakamilika kwa wakati huku akiwaonya wote watakaozembea katika majukumu yao.
Taarifa ya Mwanahabari wetu.