Sports
Martin Zubimendi Kutua Arsenal
Kilabu ya Arsenal imekubaliana na kiungo wa Real Sociadad Martin Zubimendi kuhusiana na uhamisho wa pauni milioni 51.
Raia huyo wa Uhispania mwenye umri wa miaka 26 sasa anatarajiwa kuwasili mjini London kwa vipimo vya kimatibabu baada ya kukubali kutua Emirates.
Haya yanajiri baada kuwepo kwa ripoti nchini Uhispania kwamba Real Madrid walikua wameingia kwenye kinyanganyiro cha kusaka huduma za kiungo huyo mbunifu.
Kulingana na mkali wa taarifa za Uhamisho barani ulaya Fabrizio Romano ni kwamba mchezaji huyo amekubali kuwasili London baada kukuabaliana na matakwa yake binafsi na yuko tayari kumwaga wino mkataba wa miaka mitano.
Mchezaji huyo atakua sajili wa kwanza msimu huu kwa kocha mkuu Mikel Arteta.