Sports
Martin Zubimendi Kutua Arsenal

Kilabu ya Arsenal imekubaliana na kiungo wa Real Sociadad Martin Zubimendi kuhusiana na uhamisho wa pauni milioni 51.
Raia huyo wa Uhispania mwenye umri wa miaka 26 sasa anatarajiwa kuwasili mjini London kwa vipimo vya kimatibabu baada ya kukubali kutua Emirates.
Haya yanajiri baada kuwepo kwa ripoti nchini Uhispania kwamba Real Madrid walikua wameingia kwenye kinyanganyiro cha kusaka huduma za kiungo huyo mbunifu.
Kulingana na mkali wa taarifa za Uhamisho barani ulaya Fabrizio Romano ni kwamba mchezaji huyo amekubali kuwasili London baada kukuabaliana na matakwa yake binafsi na yuko tayari kumwaga wino mkataba wa miaka mitano.
Mchezaji huyo atakua sajili wa kwanza msimu huu kwa kocha mkuu Mikel Arteta.
Sports
Florian Wirtz Sasa Mambo Nywee! Kutua Liverpool

Kilabu ya Liverpool imeafikia makubaliano na Bayern Leverkusen kuhusiana na usajili wa kiungo mbunifu Florian Wirtz uhamisho ambao ni rekodi mpya wa uhamisho Uingereza.
Timu hizo mbili zimekua kwenye mazungumzo na sasa kitita cha pauni milioni 116 imeafikiwa kwa tineja huyo mwenye umri wa miaka 22.
Raia huyo Ujerumani sasa atawasili Liverpool kwa ajili ya vipimo vya kimatibabu wiki ijayo na baadaye kutiwa wino kandarasi mpya
Inaaminika Wirtz atamwaga wino mkataba wa miaka mitano na The Reds na kuwa sajili wa pili kwa kocha Arne Slot baada ya kupata sahihi ya beki Jeremie Frimpong wa taifa la Uholanzi kwa pauni milioni 29.5.
Sports
Thomas Frank Kocha Mpya Spurs

Kilabu ya Tottenham HotSpurs ya Uingereza imemtambulisha Thomas Frank kuwa kocha mpya kumrithi Ange Postecoglou aliyepigwa kalamu mwezi jana licha kushinda kombe la Europa ligi na kilabu hiyo wakishinda Manchester United goli 1-0.
Mwalimu huyo mwenye umri wa miaka 51 amemwaga wino kwenye karatasi mktaba wa miaka mitatu na kilabu hiyo ya London Kaskazini huku kibarua cha kwanza ni kutoa kilabu hiyo kutoka nafasi ya 17 Epl na kurejesha katika ubora wake.
Raia huyo wa Denmark amekua na kilabu ya Brenford kwa miaka saba na aliwasaidia The bees kumaliza ya kumi msimu jana na alama 56 ligi ya Epl na amekua akiwindwa ni vilabu kadha wa kadha.