News

Mamlaka ya CA yasitisha matangazo ya moja kwa moja ya maandamano

Published

on

Serikali imeagiza vituo vyote vya habari vya runinga za kitaifa na radio kusitisha mara moja matangazo ya moja kwa moja ya maandamano yanayoendelea katika maeneo mbalimbali nchini.

Katika taarifa iliyotolewa na Mamlaka ya mawasiliano nchini CA na kutiwa saini na Mkurugenzi mkuu wa Mamlaka hiyo David Mugonyi, ilisema kituo chochote za habari kitakachokiuka agizo kitachukuliwa hatua za kisheria.

Mamlaka ya CA ilisema baada ya kufuatilia kwa makini matukio yote yanayoendelea katika maandamano hayo, wamebaini kwamba maandamano hayo yamekiuka kipengele cha 33 ibara ya 2 na kipengele cha 34 ibara ya kwanza ya Katiba.

CA ilidai kwamba maandamano hayo pia yameenda kinyume na kifungu cha 461 cha sheria za habari na mawasiliano nchini.

Picha kwa hisani

Wakati huo huo Mamlaka hiyo iliweka wazi kwamba itaendelea kufuatilia taarifa zote zinazopeperushwa katika runinga na Radio ili kuhakikisha zinazingatia sheria na kanuni za habari na mawasiliano.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version