Connect with us

Sports

Liverpool Kuwasilisha Ofa Mpya Kusajili Wirtz

Published

on

Mabingwa wapya wa ligi ya Epl liverpool inatarajiwa kuwasilisha ofa nyingine kusaka hudumza kiungo matata wa Ujerumani Florian Wirtz.

Hii ni Baada ya kilabu ya Bayer Leverkusen kukataa ofa ya pauni milioni 113 kutoka kwa usajli wa mchezaji huyo ambaye ameweka wazi yuko tayari kujiunga na The Reds msimu ujao.

Leverkusen imeshikilia kuwa inahitaji kitita cha pauni milioni 126 kumwachilia nyota huyo mwenye umri wa miaka 22 ambaye pia anamezewa mate na Real Madrid ya Uhispania na Manchester City wa Uingereza.

Inaaminika mchezaji huyo ndiye atakua sajili wa kwanza kwa kocha mkuu Arne Slot msimu huu wakiwa tayari kuwachiliwa nyota wake akiwemo mshmabulizi Darwin Nunez,Federico Chiesa,Harvey Elliot na Kostas Tsimiskas ambao wote wataondoka ugani Anfield.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Manchester United Ndiyo mabingwa wa ‘PREMIERE LEAGUE SUMMER SERIES’

Published

on

By

Manchester United imetwaa ubingwa wa kombe la ‘Premier League Summer Series’ kufuatia sare ya 2-2 dhidi ya Everton katika dimba la Mercedes-Benz, Atlanta, Georgia Marekani.
Michuano hiyo ya maandalizi ya msimu mpya ilishirikisha timu nne za Ligi Kuu England Man United, West Ham United, Everton na Bournemouth ambapo Mashetani hao Wekundu wamemaliza kileleni pointi 7 baada ya mechi tatu, wakishinda mechi mbili na kutoka sare mechi moja.
Kiungo Bruno Fernandes aliwaweka uongozini United dakika ya 18 kupitia mkwaju wa Penalti au Tuta kisha Iliman Ndiaye akisawazishia The Toffees dakika ya 40,United tena walichukua uongozi kupitia kwa kiungo mshambulizi Mason Mount dakika ya 69 kabila ya beki Ayden Heaven kujifunga dakika ya 75.
MSIMAMO:
1. Man UTD — mechi 3 — pointi 7
2. West Ham mechi 3 — pointi 6
3. Bournemouth mechi 3 — pointi 3
4. Everton mechi 3 — pointi 1
Continue Reading

Sports

Stars yaanza vema CHAN kwa ushindi goli 1-0 dhidi ya DR-Congo

Published

on

By

Timu ya Taifa ya Kenya (Harambee Stars) imechukua alama zote tatu kufuatia ushindi wa 1-0 dhidi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kwenye mchezo wa kwanza wa Kundi B wa kombe la Mataifa Afrika CHAN 2024 katika dimba la Moi Sports Centre, Nairobi.
Goli hilo la kipekee lilitiwa wavuni na kiungo mshambulizi Austine Odhiambo dakika 45 kipindi cha kwanza.
Rais William Ruto ambaye alifuatilia mechi hiyo uwanjani alitembelea kikosi katika chumba cha kubadilisha na kukabidhi ahadi yake ya shilindi milioni moja kwa kila mchezaji baada ya ushindi huo.
Stars wamekwea kileleni mwa kundi A na alama Tatu kundi ambalo pia lina Morocco,Zambia na Angola Mechi ijayo ya Stars ni dhidi ya Angola ni Agosti 7.
Continue Reading

Trending