Business

KPA kuekeza kwenye miradi muhimu

Published

on

Mamlaka ya bandari ya nchini (KPA) imesema itaendelea kuekeza katika miradi muhimu ya miundombinu ili kukidhi ongezeko la mahitaji ya usafirishaji wa mizigo kupitia reli, baharini na barabara.

Meneja mkuu wa operesheni za mizigo katika KPA, Dkt. Sudi Mwasinago, alisema kuwa uwekezaji huo umechangia kwa kiasi kikubwa kuongeza ufanisi katika shughuli za bandari, hasa kufuatia uimarishaji wa mifumo ya kiutendaji na ununuzi wa vifaa vya kisasa.

Akizungumza katika kikao kilichowakutanisha wadau kutoka KPA, shirika la reli nchini (KRC), na maafisa kutoka Etihad Rail ya Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE), Dkt. Mwasinago alisema kuwa ushirikiano kati ya mashirika hayo ni hatua muhimu katika kuimarisha sekta ya usafirishaji nchini.

Dkt. Mwasinago, alisema KPA inaendelea kujenga mazingira bora ya biashara kwa kuunganisha bandari na miundombinu mingine ya usafiri, ikiwa ni pamoja na reli ya kisasa ya SGR na barabara kuu, ili kuhakikisha mchakato wa usambazaji wa bidhaa unakuwa mwepesi na wenye tija.

Aidha, kampuni ya Etihad Rail, ilionyesha nia ya dhati ya kushirikiana na Kenya katika uendelezaji wa mtandao wa reli wa kisasa ili kuboresha viwango vya usafiri wa reli nchini, sambamba na kukuza biashara ya kimataifa kupitia bandari ya Mombasa.

Taarifa ya Mwanahabari

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version