National News
Kocha wa Stars Ashukuru Mashabiki
Mkufunzi wa Timu ya taifa Harambee stars Benni McCarthy amesema kwamba walikutana na mpinzani Bora Gabon katika mechi ya kufuzu kombe la Dunia ugani Nyayo siku ya Jumapili.
Haya yanajiri baada ya stars kupokea kichapo Cha magoli 2-1 dhidi ya The panthers na mwalimu ana amini Gabon tayari wa kikosi Bora kuliko stars na Hilo lilionekana.
“Ni kweli tumekutana na timu Bora ambayo tayari imenjeka kwa muda sisi tumefanya mazoezi siku mbili pekee kinyume na wao.”
Kwa upande wake kocha wa Gabon Thierry myomou amesema kwamba mipango ilifanya Kazi kwani Lengo lao lilikua Moja tu kupata ushindi ama sare ugenini kwa bahati mzuri wakaondoka na ushindi.
“Tulikua na Lengo LA kushinda mechi hii kutokea mwanzo ama kama iwe vigumu tupate sare kwa bahati mzuri tumepata alama zote tatu ni furaha kwetu kwani ulikua ni mechi ngumu mbele ya mashabiki wa nyumbani.
“Hata hivyo McCarthy ameshukuru mashabiki wengi waliokitokeza kuipa msukumo stars akikiri tangu akiwa mchezaji hajaona uwanja ukiwa umefurika hivyo akitaka mailtaifa mengine barani Afrika kuiga Hilo.
“Nichukue fursa kushukuru mashabiki wameonyesha jinsi gani wana upendo kwa timu yetu inasikitisha hatujawapa tabasamu wanaporudi nyumbani ila niwahakikishie nanjenga timu ambayo itaeletea Raha mashabiki wa nyumbani siku za usoni.”
Stars kwa Sasa wanaketi nafasi ya nne kundi F wakiwa na alama sita , Ivory coast wako kileleni na alama 16 baada ya ushindi dhidi ya Gambia nayo Gabon ni ya pili na alama 15 Burundi ni ya tatu na lama 7.