News
Kenya Yatoa ufadhili wa Asilimia 20 kwa WHO
Kenya imejitolea kuongeza ufadhili wake kwa Shirika la Afya duniani WHO kwa asilimia 20 katika kipindi cha miaka 4 ijayo.
Waziri wa Afya nchini Aden Duale ameyasema hayo wakati wa Kongamano la 78 la Afya duniani linaloendelea mjini Geneva nchini Uswizi, ambapo amesisitiza haja ya serikali ya Kenya kujitolea katika kuboresha sekta ya afya ulimwenguni.
Waziri Duale amesisitiza umuhimu wa ufadhili endelevu kwa Shirika la Afya duniani WHO, akisema licha ya bajeti kurekebishwa na kuweka ufadhili huo mdogo pia utasaidia sekta ya afya.
Waziri Duale ameangazia dhamira ya serikali ya Kenya ya kuhakikisha wananchi wananufaika na huduma za afya kwa wote UHC, kuimarishwa kwa ufadhili wa afya na kuendeleza miundombinu ya afya ya kidijitali ili kuendesha sera inayotumia data.
Kwa upande wake Mkurugenzi mkuu wa WHO Dkt Tedros Adhanom Ghebreyesus amepongeza kujitolea kwa mataifa wanachama katika kufadhili WHO, akisema ahadi zilizotolewa na mataifa hayo zitachangia kuimarika kwa sekta ya afya duniani.