News

KEMNAC, yaunga mkono taifa la Tanzania kutoruhusu Wanaharakati wa Kenya

Published

on

Baraza kuu la mashauri ya Waislamu nchini KEMNAC limeunga mkono taifa la Tanzania kwa kutoruhusu Wanaharakati wa kijamii na baadhi ya viongozi kutoka Kenya kuingilia siasa za taifa hilo.

Mwenyekiti wa baraza hilo Sheikh Juma Ngao, alisema Tanzania kuna amani na utulivu mkubwa ikilinganishwa na mataifa mengine ya Afrika mashariki.

Sheikh Ngao, aliwataka vijana wanaotengeneza maudhui na semi za kutisha na kumkejeli Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kukoma mara moja, akisisitiza kuwa ni kumkosea heshima na kumdhalilisha kiongozi huyo bila sababu za msingi.

Sheikh Ngao alisema taifa la Kenya limejaa ukabila na chuki za kisiasa tofauti na na taifa la Tanzania ambalo linajulikana kuwa taifa lenya amani na uzalendo huku akiwataka wakenya kuimarisha umoja na mshikamano kabla ya kuenda kutafutia amani nchi zengine.

“Tanzania tangu ipate uhuru wake, jeshi lake halijathubutu kupindua nchi hapa waliothubutu, hakujaandamanwa kuvamia bunge na kulichoma hapa ilifanyika, hakujapiganwa mpaka kukapatikana Waziri mkuu wa nchini kule kulipatikana Waziri mkuu kisheria, kwa hivyo Kenya huweze kuwafundisha watu wa Tanzania mambo ya Amani”, alisema Sheikh Ngao.

Kwa upande wake, Abubakar Amin Al’alawi, ambaye ni Naibu Mwenyekiti wa Baraza hilo, aliwataka viongozi wa kidini, kijamii, na wazazi kuwaelimisha vijana na watoto wao kuhusu maadili mema ili kuepuka chuki miongoni mwa mataifa haya mawili.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version