News
Imarika Sacco yazindua kampeni ya Ekeza na ushinde–Imarika gari promotion
Wateja na wanachama wa shirika la uekezaji na mikopo la Imarika Sacco walijumuika na maafisa na shirika hilo katika maeneo mbali mbali kaunti ya Kilifi kwenye kampeni ya kuwahamasisha kuhusu kuekeza na kujishindia zawadi chungu nzima.
Vivile vile wateja hao pamoja na mashabiki wa kituo hiki cha Coco fm walipata fursa ya kukutana na watangazaji moja kwa moja katika msafara ulioanza eneo la Gongoni, kuelekea Malindi, Gede, Watamu, Mastangoni na kutamatika eneo la Mkoroshoni Mjini Kilifi.
Kulingana na afisa mthibiti wa akiba Agricola Ngeti kutoka shirika la Imarika Sacco, kampeni hiyo iliyopewa jina Ekeza na ushinde–Imarika gari promotion iling’oa nanga kuanzia tarehe saba mwezi wa Julai, 2025 hadi tarehe 30, Novemba 2025.
Ngeti alisihi wanachama na wale ambao hawajajisajili na shirika hilo kufanya hivyo na kuekeza zaidi, ili kupata fursa ya kujishindia zawadi.
“Kwa mwanachama yeyote ambaye ambaye atataka kwa hili shindano anafaa aekeze kiwango cha chini cha shilingi 1,000, lakini inatakikana ile pesa ambayo unaekezxa kila mwezi iwe zaidi ya chenye mwanachama ataekeza ndio aingine kwenye shindano, zaidi anavyoendelea kuekeza ndio anakaribia kuwa mshindi, kwa wale wanachama ambao watakuwa watatu kwa washindi wa wiki watashinda 5,000 wale washindi wa mwezi tutachukua 2,000 tutapeleka kwa share capital, halafu mshindi wa kwanza atapewa gari, wapili atapewa tuktuk na watatu atapewa pikipiki”, alisema Bi Ngeti
Baadhi ya waliojitokeza kwenye msafara wa Imarika Sacco na Coco Fm Gongoni.
Ngeti aliongeza kuwa mesema lengo kuu la kampeni hiyo ni kusaidia wanachama kuekeza zaidi na kufaidika na mikapo.
“Tunasaidia wanachama wetu waekeze zaidi wapate mikopo na sisi kama Sacco tuwe na pesa nyingi ambazo tunaweza kukopesha wanachama wetu”, aliongeza Ngeti
Umati uliojitokeza kwenye kampeni ya Ekeza na ushinde–Imarika gari promotion eneo la mkoroshoni Kilifi.
Baadhi ya wateja waliojisajili na shirika hilo akiwepo Samuel Kifalu wameeleza matumaini na kunufaika na huduma za uekezaji katika shirika hilo la Imarika Sacco.
“Nimefungua akaunti nataka kujiekezea ili kuanza biashara, nazieka kwenye akaunti ikifika kiwango cha kupewa mkopo nianze biashara ya kujiendeleza, Imarika Sacco iko sawa, kwa mwezi natarajia kuweka kama shilingi 5,000, nataka kushinda hata kama nigari ama tuktuk au pikipiki”, Alisema Kifalu.
Taarifa ya Joseph Jira