News
Imarika Sacco yazindua kampeni ya Ekeza na ushinde–Imarika gari promotion

Wateja na wanachama wa shirika la uekezaji na mikopo la Imarika Sacco walijumuika na maafisa na shirika hilo katika maeneo mbali mbali kaunti ya Kilifi kwenye kampeni ya kuwahamasisha kuhusu kuekeza na kujishindia zawadi chungu nzima.
Vivile vile wateja hao pamoja na mashabiki wa kituo hiki cha Coco fm walipata fursa ya kukutana na watangazaji moja kwa moja katika msafara ulioanza eneo la Gongoni, kuelekea Malindi, Gede, Watamu, Mastangoni na kutamatika eneo la Mkoroshoni Mjini Kilifi.
Kulingana na afisa mthibiti wa akiba Agricola Ngeti kutoka shirika la Imarika Sacco, kampeni hiyo iliyopewa jina Ekeza na ushinde–Imarika gari promotion iling’oa nanga kuanzia tarehe saba mwezi wa Julai, 2025 hadi tarehe 30, Novemba 2025.
Ngeti alisihi wanachama na wale ambao hawajajisajili na shirika hilo kufanya hivyo na kuekeza zaidi, ili kupata fursa ya kujishindia zawadi.
“Kwa mwanachama yeyote ambaye ambaye atataka kwa hili shindano anafaa aekeze kiwango cha chini cha shilingi 1,000, lakini inatakikana ile pesa ambayo unaekezxa kila mwezi iwe zaidi ya chenye mwanachama ataekeza ndio aingine kwenye shindano, zaidi anavyoendelea kuekeza ndio anakaribia kuwa mshindi, kwa wale wanachama ambao watakuwa watatu kwa washindi wa wiki watashinda 5,000 wale washindi wa mwezi tutachukua 2,000 tutapeleka kwa share capital, halafu mshindi wa kwanza atapewa gari, wapili atapewa tuktuk na watatu atapewa pikipiki”, alisema Bi Ngeti
Baadhi ya waliojitokeza kwenye msafara wa Imarika Sacco na Coco Fm Gongoni.
Ngeti aliongeza kuwa mesema lengo kuu la kampeni hiyo ni kusaidia wanachama kuekeza zaidi na kufaidika na mikapo.
“Tunasaidia wanachama wetu waekeze zaidi wapate mikopo na sisi kama Sacco tuwe na pesa nyingi ambazo tunaweza kukopesha wanachama wetu”, aliongeza Ngeti
Umati uliojitokeza kwenye kampeni ya Ekeza na ushinde–Imarika gari promotion eneo la mkoroshoni Kilifi.
Baadhi ya wateja waliojisajili na shirika hilo akiwepo Samuel Kifalu wameeleza matumaini na kunufaika na huduma za uekezaji katika shirika hilo la Imarika Sacco.
“Nimefungua akaunti nataka kujiekezea ili kuanza biashara, nazieka kwenye akaunti ikifika kiwango cha kupewa mkopo nianze biashara ya kujiendeleza, Imarika Sacco iko sawa, kwa mwezi natarajia kuweka kama shilingi 5,000, nataka kushinda hata kama nigari ama tuktuk au pikipiki”, Alisema Kifalu.
Taarifa ya Joseph Jira
News
IEBC inaendelea kutambua vituo vya kusajili wapiga kura

Maafisa wa tume ya uchaguzi na mipaka nchini IEBC wamesema wanaendelea na zoezi la kutambua sehemu za kuweka vituo vya kusajili wapiga kura hasa maeneo ya mashinani.
Afisa msimamizi wa tume ya IEBC eneo bunge la Ganze kaunti ya Kilifi, Mohammed Bahero Aboud alisema juhudi hizo ni kuhakikisha zoezi la usajili wapiga kura litakaloanza rasmi Septemba 29, mwaka huu linafaulu.
Akizungumza mjini Kilifi, Bahero alisema tume hiyo inatumia mbinu mpya ya kutambua vituo vya jadi vya usajili wapiga kura na kuweka vituo vipya kulingana na mapendekezo ya sheria.
Wakati huo huo alidokeza kwamba tume ya IEBC imekuwa ikihamashisha wakenya kutokubali kushawishiwa na wanasiasa na kujisajili katika maeneo yasiokuwa yao hasa msimu huu ambao zoezi hilo linakaribia kuanza.
Taarifa ya Joseph Jira
News
Kaunti ya Mombasa kukumbatia matumizi ya mfumo wa miale ya jua

Serikali ya kaunti ya Mombasa imesema imeanza kutekeleza mpango wa kutumia nishati mbadala katika vituo vyote vya huduma za kaunti, kwa kuanza na mabadiliko ya mfumo wa taa hadi kutumia umeme wa miale ya jua.
Kwa mujibu wa waziri wa kawi, rasilimali asili na ustahimilivu dhidi ya mabadiliko ya tabianchi kaunti ya Mombasa, Emily Achieng, hatua hii inalenga kupunguza gharama za matumizi ya umeme na kuhimiza matumizi ya nishati safi na rafiki kwa mazingira.
Mbali na hilo, waziri huyo alisema kaunti inaendelea kuweka vifaa maalum vya kupima ubora wa hewa katika maeneo mbalimbali ya mji na ndani ya taasisi za umma.
Lengo ni kupata ushahidi wa kisayansi kuhusu kiwango cha uchafuzi wa hewa, na kuchukuliwa kwa hatua za kisheria kwa wanaokiuka sheria.
Vifaa hivyo tayari vimewekwa katika hospitali ya rufaa ya Coast General na baadhi ya shule ikiwa ni sehemu ya mpango wa muda mrefu wa kaunti, kujenga ustahimilivu dhidi ya madhara ya mabadiliko ya tabianchi.
Mikakati hiyo pia itasaidia kaunti katika kufanya maamuzi kuhusu maeneo yanayofaa kuwekwa biashara fulani, ili kulinda wananchi dhidi ya maradhi yanayosababishwa na uchafuzi wa hewa.
Taarifa ya Mwanahabari wetu.