Uncategorized
Douglas Kanja, Mohammed Amin wakosa kufika mahakamani.
Siku kumi baada ya mwanablogu Ndiang’ui Kinyagia kutoweka, kesi ya kumtaka inspecta jenerali wa polisi Doglas Kanja kueleza alipo mwanablogu huyo iliendelea kusikilizwa katika mahakama ya Milimani jijini Nairobi.
Inspecta jenerali wa polisi Douglas Kanja pamoja na mkurugenzi wa idara ya upelelezi wa makosa ya jinai DCI Mohammed Amin walikosa kufika katika mahakama kama ilivyo amriwa hapo awali.
Haya yanajiri huku maafisa wa DCI wakiongozwa na mkurugenzi wa DCI wakiiambia mahakama siku ya jumatatu 30 juni 2025 kwamba hawakumkamata mwanablogu huyo.
Kwa upande wake Jaji Chacha Mwita aliwataka wawili hao kuhakikisha wanaeleza alipo mwanablogu huyo.
“Hakuna vile mtu anaweza toweka ghafla na hajulikani alipo, hatutaki maneno mengi tunachotaka ni huyu mtu ako wapi mleteni mbele ya mahakama awe hai au mfu tunachotaka ni huyu mtu yupo wai?”,aliuliza jaji Chacha Mwita.
Viongozi mbalimbali akiwemo kinara wa chama cha PLP Martha Karua, mbunge wa Embakasi Mashariki Paul Ongili Owino maarufu Babu Owino miongoni mwa viongozi wengine walihudhuria kikao cha kesi hiyo huku Karua akisema kwamba, wawili hao wameonyesha utovu mkubwa na nidhamu kwa kukiuka amri ya mahakama.
Ikumbukwe kwamba mwanablogu Kinyagia alikamatwa tarehe 21 juni 2025 kwa kosa la uhalifu wa kimitandao ikiwa ni kuchapisha ratiba ya maandamano yaliyofanyika Jumatano tarehe 25 Juni 2025.
Taarifa ya Elizabeth Mwende