News
David Maraga amfokea mkurugenzi wa mashtaka ya umma
Jaji mkuu mstaafu David Maraga amefokea ofisi ya mkurugenzi wa mashtaka ya umma kwa kuwashtaki kwa makosa ya ugaidi vijana waliokamatwa wakati wa maandamano.
Maraga alisema hatua hiyo inawadhulumu vijana hao ambao wamesalia korokoroni wakisubiri kesi yao kuamuliwa.
Maraga pia aliaka kesi hizo zitupiliwe mbali akisema hazina msingi, akidai hatua hiyo ni utumizi mbaya wa sheria kwa madai ya kukabiliana na magaidi, ilihali walioshtakiwa walikuwa wakishinikiza uongozi bora nchini.
Maraga pamoja na wanaharakati wa kutetea haki za binadam walimtaka mkurugenzi wa mashtaka ya umma Renson Ingonga kuwajibika na kutupilia mbali kesi hizo na kuwaruhusu washukiwa kuendelea na maisha yao.
Taarifa ya Joseph Jira