Sports
City Yasajili Wachezaji Watatu
Kilabu ya Manchester City imetangaza kukamilisha uhamisho wa wachezaji watatu tayari kwa msimu mpya baada ya kukamilisha vipimo vya kimatibabu.
Wachezaji hao watatu ni pamoja na beki Rayan Ait -Nouri kutoka kilabu ya Wolves kwa pauni milioni 31 mchezaji huyo tayari amepasi vipimo vya kimatibabu na kumwaga wino mkataba wa miaka mitano na The Citizens.
Wachezaji wengine ni Tijjani Reinders ambaye amejiunga na kilabu hiyo kwa pauni milioni 55 akitokea kilabu ya AC Milan ya Italia kwa mkataba wa miaka mitano pia.
Timu hiyo pia imekamilisha usajili wa winga wa taifa la Ufaransa na kilabu ya Lyon ya Ufaransa Rayan Cherki ambaye anajiunga na kilabu hiyo kwa pauni milioni 45 na ametia wino mkataba wa miaka mitano.