News

Biwott: Polisi waendelea kuwasaka waumini wenye itikadi potovu

Published

on

Kamanda wa Polisi kaunti ya Kilifi Josephat Biwott amepongeza juhudi za wakaazi wa kaunti hiyo kwa kuwa na ushirikiano mwema na asasi za usalama.

Biwott amesema ni kupitia ushirikiano huo ambapo oparesheni ya kuwanasa waumini wa dini potofu eneo la Binzaro, kilomita chache kutoka eneo la Shakahola imefanikiwa kutokana na juhudi za wakaazi kutoa taarifa kwa maafisa wa usalama.

Akizungumza na Coco Fm, Biwott alithibitisha kwamba eneo la Chakama lipo chini ya ulinzi wa polisi.

Biwott alidhitisha kuwa washukiwa 11 tayari wamekamatwa na wamefikishwa Mahakamani Jumanne 22 Julai 2025 mbele ya Hakimu Mwandamizi Joy Wesonga na wataendelea kuzuiliwa katika kituo cha Polisi mjini Malindi.

Biwott aidha alisema maafisa wa usalama wanachunguza iwapo washukiwa hao walienda msituni wakiwa na watoto.

“Nawashukuru wananchi wetu hasa wakaazi wa Binzaro, kwa kutueleza kwa mapema sana kuhusu yale mambo yalikua yanaendelea huko kwa vile wametueleza tumefaulu kuokoa wale ambao tumeokoa na wanaoendelea dini hiyo tumewakamata na wamefikishwa mahakamani”. …alisema Biwott, kwa njia ya simu.

Tarifa ya Elizabeth Mwende

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version