Sports
Gyokeres Sasa Ni Mali Ya Arsenal
Klabu ya Arsenal imefikia makubaliano na Sporting Lisbon juu ya kumsajili mshambuliaji Victor Gyokeres kwa ada ya uhamisho ya Euro milioni 63.5 na nyongeza ya milioni 10.
Gyökeres, 27, raia wa Sweden anatarajiwa kusaini mkataba wa miaka mitano utakaombakisha kwa Washika Mitutu hao mpaka Juni 2030.
Kumekuwepo na sintofahamu kuhusiana na uhamisho huo baada ya Kilabu ya Manchester United kujaribu kupokonya Arsenal Mshambulizi huyo Ila Mshambulizi huyo alisalia kwamba anataka Arsenal pekee.
Mchezaji huyo anakua sajili wa tano kwa The Gunners baada ya usajili wa kipa Kepa Arrizabalaga,kiungo Martin Zubimendi,Christian Norgard na Mosquera.