News
Wazazi na Walimu wahimiza Wanafunzi kujiunga na Skauti.
Wazazi na walimu kaunti ya Kwale wameshinikiza kuhimiza wanafunzi kujiunga zaidi na kundi la maskauti kutokana na idadi ndogo ya maskauti kaunti hiyo.
Akizungumza wakati wa kongamano la maskauti la ngazi za kaunti linalofanyika katika shule ya msingi ya Kinango kaunti ya Kwale, Kamanda wa skauti wa gatuzi dogo hilo Mambo Tsuma alieleza kuwa changamoto hiyo ya idadi ndogo inaendelea kuhatarisha uwepo wa skauti.
Baadhi ya wanafunzi maskauti kaunti ya Kwale
Kwa upande wake Mwalimu Abbas Kanyalo,aliitaka idara ya elimu ikishirikiana na viongozi wengine kukumbatia swala la skauti katika shule zote nchini na kuipa skauti kipau mbele.
Kongamano hilo la siku 3 lilijuisha shule 58 kutoka eneo hilo la Kwale ikiwemo shule za sekondari, sekondari msingi, shule za msingi na shule za wanafunzi wenye uwezo maalum.
Taarifa ya Mwanahabari.