News

Maafisa wa Polisi Wamewakamata Wahalifu 9, Mtwapa.

Published

on

Maafisa wa usalama eneo la pwani wanasema wamewakamata wanaume 9 wa umri kati ya miaka 26 hadi 30 kwa tuhuma za wizi eneo la Mtwapa kaunti ya Kilifi.

Kulingana na polisi washukiwa walikamatwa na mali ya uizi yenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 7 katika nyumba wanamoishi.

Kamanda wa polisi hapa pwani Ali Nuno alisema maafisa wa polisi wamefanikiwa kupata magari nane yanayodaiwa kuwa ya wizi, baadhi yakiaminika kutumika na washukiwa kutekeleza shughuli hizo.

Nuno alidokeza washukiwa wamekuwa wakiwawinda watu wanaotoka kutoa pesa kwenye benki na kuwaibia kwa kutumia vifaa maalumu vya kufungua magari wakati wanapoziwacha pesa hizo ndani ya gari.

Nono vile vile alidokeza kuwa baadhi ya washukiwa waliokamatwa ni wezi sugu na ambao wanaripoti za kihalifu zilizoripotiwa tangu mwaka 2017 katika mahakama ya Mombasa.

Taarifa ya Joseph Jira

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version