Sports
Kilabu ya Chelsea Ndiyo Mabingwa wa Conference League
Kilabu ya Chelsea ya Uingereza imekua ya kwanza kushinda taji la Kilabu Bingwa Ulaya,taji la Uefa Europa ligi,Uefa Supa Cup na Taji la Conference ligi katika historia ya mataji hayo barani Ulaya.
Hii ni baada ya The Blues kutia darasani kabla ya kuchachafya kilabu ya Real Betis ya Uhispania kichapo cha magoli 4-1 uwanjani majeski stadium,Poland fainali ya conference ligi.
Kilabu ya Real Betis walitanguliwa kufunga kupitia winga matata wa taifa la Morocco Abde Elizouzoli dakika ya 9 Lakini chelsea walikua na jambo lao wakirejea kwa kishindo kipindo cha pili kupitia magoli ya kiungo MuArgentina Enzo Fernandez dakika 65,kisha Mshambulizi wa taifa la Senegal Nicholas Jackson akipachika wavuni goli la pili dakika ya 70,
winga matata wa Manchester United Muingereza Jadon Sancho aliongeza la tatu dakika ya 70,huku Kiungo mkabaji Moses Caicedo akizika Betis kwa chuma cha nne kunako dakika ya 93 na kunyakua kombe hilo.
Kombe hilo ni taji la kwanza kwa kocha Enzo Maresca kilabuni humo na hakuficha furaha yake baada ya kuwapa furaha mashabiki wa The Blues.