Connect with us

Sports

Kilabu ya Chelsea Ndiyo Mabingwa wa Conference League

Published

on

Kilabu ya Chelsea ya Uingereza imekua ya kwanza kushinda taji la Kilabu Bingwa Ulaya,taji la Uefa Europa ligi,Uefa Supa Cup na Taji la Conference ligi katika historia ya mataji hayo barani Ulaya.

Hii ni baada ya The Blues kutia darasani kabla ya kuchachafya kilabu ya Real Betis ya Uhispania kichapo cha magoli 4-1 uwanjani majeski stadium,Poland fainali ya conference ligi.

Kilabu ya Real Betis walitanguliwa kufunga kupitia winga matata wa taifa la Morocco Abde Elizouzoli dakika ya 9 Lakini  chelsea walikua na jambo lao wakirejea kwa kishindo kipindo cha pili kupitia magoli ya kiungo MuArgentina Enzo Fernandez dakika 65,kisha Mshambulizi wa taifa la Senegal Nicholas Jackson akipachika wavuni goli la pili dakika ya 70,

winga matata wa Manchester United Muingereza Jadon Sancho aliongeza la tatu dakika ya 70,huku Kiungo mkabaji Moses Caicedo akizika Betis kwa chuma cha nne kunako dakika ya 93 na kunyakua kombe hilo.

Kombe hilo ni taji la kwanza kwa kocha Enzo Maresca kilabuni humo na hakuficha furaha yake baada ya kuwapa furaha mashabiki wa The Blues.

 

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

INZAGI Bado Yuko Saana Inter.

Published

on

By

Uongozi wa klabu ya Inter Milan uko radhi kurefusa mkataba wa kocha Simone Inzaghi licha ya kufeli
kutwaa taji la klabu bingwa Uropa siku ya jumamosi.
Rais wa Inter Giuseppe Marotta, ameelezea Imani kwa uongozi wa Kocha Inzaghi, licha ya kibano cha
magoli 5-0 klabu hiyo ilipokea katika fainali ya klabu bingwa uropa dhidi ya Paris Saint-Germain
(PSG) na kupoteza fainali ya pili mtawalia, ya kwanza ikiwa msimu wa mwaka 2022/2023 mikononi
mwa Manchester City.
Mkataba wa Inzaghi unakamilika mwezi juni mwaka ujao ila Marotta, amesisitiza kuwa mazungumzo na
kocha huyo yataanza hivi karibuni, baada ya tetesi kuwa Inzaghi anajiondoa Inter na hatakuwepo
kuitayarisha kwa ajili ya msimu ujao.
“Kushindwa katika fainali hauna msukumo wowote, inzaghi ana mkataba wa mwaka mmoja Zaidi na
tuliamua kukutana naye juma hili” Alisema Marotta katika kikao na wanahabari baada ya fainali ya klabu
bingwa uropa huko Munich Ujerumani. “Mafanikio yote na makali ya klabu yanayoonekana ni kwa ajili
ya uwezo na utaalam wake,Tutafurahia iwapo yuko radhi kuendelea na kazi.”

Continue Reading

Sports

Inter Wapiga Msamba, PSG Wakivuma Uefa.

Published

on

By

Klabu ya Paris Saint-Germain (PSG) ndio mabingwa wa Klabu bingwa Uropa baada ya kuilaza Inter-Milan magoli 5-0 Jumamosi usiku, katika fainali iliyochezewa katika uwanja wa Allianz Arena jijini Munich, Ujerumani.

Mvua ya magoli ilianzishwa na beki Ashram Hakimi dakika ya 12, kabla ya kiungo mshambuliaji wa PSG Desire Doue kuongeza bao la pili dakika ya 20, na goli la tatu katika dakika ya 60 huku goli la nne na tano likifungwa katika dakika ya 73 na 86 mtawalia.

Kocha wa PSG Luis Enrique amewasifia wachezaji wake sawa na mashabiki waliojitokeza kuishangilia klabu hiyo, ikijipatia taji kuu la kwanza Uropa baada ya kuingia fainali ya mashindano haya mara mbili kwa kipindi cha miaka mitano.

“Nafurahia sana ushindi huu” Alisema Kocha Enrique. “Fainali imekua na hisia sana hasa nilipoona bango la mashabiki kuhusu familia yangu”

Kikosi hichi changa cha PSG kimeafikia kile ambacho wachezaji nyota kama Lionell Messi, Neymar, Zlatan Ibrahimovich, Beckam na Kylian Mbappe walishindwa kutekeleza wakivalia jezi ya PSG

Paris Saint-Germain (PSG) imekua klabu ya pili Ufaransa kushinda taji la Klabu bingwa Uropa baada ya Marseille mwaka 1993.

Continue Reading

Trending