News
Manchester United Ndaani Ya Fainali Europa
Miamba wa Uingereza kilabu ya Manchester United imetinga kwenye fainali ya Europa ligi msimu huu kishindo bila kupoteza hata mechi moja.
Haya yanajiri baada ya vijana wa Kocha Ruben Amorim kuinyuka kabla ya kutandika sawa sawa kilabu ya Athletico Bilbao kichapo cha magoli 4-1 na jumla ya magoli 7-1
Wageni walichukua uongozi wa mapema kupitia kiungo Mikel Juregizer dakika ya 31 kipindi cha kwanza ,hata hivyo mashetani wekundu hao walirejea kwa moto wa radi kipindi cha pili wakijipatia magoli yao kupitia kiungo muingereza Mason Mount dakika ya 71 kabila ya Kiungo Casemiro kuongeza la pili dakika ya 80 huku mshmabulizi Rasmus Hojlund akicheka na nyavu dakika ya 85 na Mount Kuongeza lake la Pili na la nne kwa United dakika ya 93.
Katika matokeo mengine Tottenham Hotspurs walinyuka Bodo/Glimt 2-0 na jumla ya magoli 5-1 na sasa fainali ni kati ya timu za Manchester United na Spurs Ugani San Mames Uhispania Mei 21.