Sports
Thomas Frank Kocha Mpya Spurs
Kilabu ya Tottenham HotSpurs ya Uingereza imemtambulisha Thomas Frank kuwa kocha mpya kumrithi Ange Postecoglou aliyepigwa kalamu mwezi jana licha kushinda kombe la Europa ligi na kilabu hiyo wakishinda Manchester United goli 1-0.
Mwalimu huyo mwenye umri wa miaka 51 amemwaga wino kwenye karatasi mktaba wa miaka mitatu na kilabu hiyo ya London Kaskazini huku kibarua cha kwanza ni kutoa kilabu hiyo kutoka nafasi ya 17 Epl na kurejesha katika ubora wake.
Raia huyo wa Denmark amekua na kilabu ya Brenford kwa miaka saba na aliwasaidia The bees kumaliza ya kumi msimu jana na alama 56 ligi ya Epl na amekua akiwindwa ni vilabu kadha wa kadha.