Mariakani FC ya Kaloleni ndiyo mabingwa wa Makala ya kwanza Cocofm Supercup

Mariakani FC ya Kaloleni ndiyo mabingwa wa Makala ya kwanza Cocofm Supercup

MARIAKANI FC MABINGWA

Timu ya soka ya vijana ya Mariakani fc ni Moja wapo ya timu zinazo kua Kwa kasi sana kutoka wadi ya Kaloleni, Kaunti ndogo ya Kaloleni – Kilifi.

Ni timu ambayo inatia fora viwanjani sio tu Kwa mashabiki wake kutoka eneo la Kaloleni bali kuvutia umaarufu kote katika kaunti ya Kilifi.

Kwa sasa timu hiyo inashiriki ligi ya kimaeneo baada ya kushushwa daraja ligi ya divisheni ya pili ukanda wa Pwani kaskazini, chini ya kocha mkuu.

Hivi majuzi timu hiyo ilishiriki katika kombe maalum la CocoFm Super Cup makala ya kwanza yaliyofanyika Jumanne ya Disemba 16 na Jumatano ya Disemba 17 katika uga wa Mmkoroshoni mjini Kilifi ambapo iliibuka na kombe hilo.

Kombe hili ambalo lilidhaminiwa moja Kwa moja na kituo cha utangazaji cha Coco fm Kwa ushirikiano na Wakfu wa George Kithi, linalenga kukuza zaidi talanta kutoka nyanjani haswa timu kama hii ya Mariakani FC.

Kikosi hicho kinchonolewa na Godfrey Gari kilianza mashindano hayo kwa kishindo baada ya kuinyuka klabu ya Interdebaso ya kaunti ndogo ya Kilifi Kaskazini magoli 4-2 kupitia matuta au penalti , baada ya sare ya goli 1-1 muda wa kawaida.

Pia Mariakani waliibuka na ushindi wa 4-3 kupitia matuta au penalty baada ya sare ya magoli 2-2 katika mchezo wa nusu fainali ugani Mkroshoni.rama chengo na issa mwachiwayo

Katika fainali vijana hao walitumia mbinu ile ile ikizamisha meli Beach Bay marufu kama the Worriors of the Bay magoli 4-2 kupitia mikwaju ya matuta baada ya sare tasa muda wa kawaida wakifunga penalty zote.

Penalti zikifungwa na Munga Mwatuya,mwaringa Birya,Rama Chango,Julius Timona.

Mariakani walijishindia shilindi laki 2 kwa kuwa bingwa pamoja na kombe na medali rasmi katika hafla ya kihistoria uwanja ukiwa umefurika.

 

Kikosi cha Mariakani FC

1 Ayanga kayo

2 Nyawa mrinzi

3 joash omondi
4 kasimu munga
5 hamadi Alfan
6 James ndege
7 Noverty onyango
8 Munga mwadzuwa
9 Julius timona
10 Rama karisa
11 mwaringa biryani
12 Isa mwachiwaya
13 Ramadhan madela
14 Ramadhan mwahanje
Kocha mkuu; Godfrey Gari
Mki FC vs dabaso 1-1
Penaitis 4-2
Matanomane FC vs mki 2-2
Penalty 3-4
Mki FC vs Beach bay 0-0 penalty 4-2