Sports
Sane Sasa Ni Mali Ya Galatasaray
Ni rasmi aliyekua kiungo wa Manchester cityna Bayern Munich ya Ujerumani Leroy Sane amekamilisha uhamisho wake katika kilabu ya Galatasaray ya Uturuki bila ada yoyote.
Sane mwenye umri wa miaka 30 amepasi vipimo vya kimatibabu baada ya kuwasili mjini Istanbul alipolakiwa na mshabiki wengi wa kilabu hiyo anapojiunga na mabingwa hao wa ligi ya Uturuki.
Mchezaji huyo alijiunga na Bayern Munich msimu wa mwaka 2020 akitokea Mancity kwa mkataba wa miaka mitano na amefanikiwa kufunga magoli 61 katika mechi 220 ambazo amechezea timu hio.
Kiungo huyo pia amekua nguzo muhimu kwa timu ya taifa la Ujerumani akifanikiwa kufunga magoli 14 katika mechi 70 ambazo ameshirikisha katika timu hiyo.
Sane ni miongoni mwa wachezaji walionyeshwa mlango na kilabu ya Bayern Munich kwa msimu mpya.