Sports

Sancho Kurejea Manchester United.

Published

on

Kilabu ya Chelsea imelipa ada ya pauni milioni 5 na kuvunja mkataba kati yao na winga wa Manchseter United Jadon Sancho ambaye amekuwepo kilabuni humo japo kwa mkopo.

The Blues walikua tayari kulipa ada ya pauni milioni 25 kwa Mashetani Wekundu kupata sahihi ya winga huyo ila matakwa ya binafsi ya mchezaji huyo ikiwemo mshahara wake wa kila wiki ilizua kutoelewana na badaye kilabu hiyo kubaki na si lingine ila kuvunja mkataba huo.

Sancho mwenye umri wa miaka 26 amekua na wakati mzuri ugani Stamford Bridge akisaidia Chelsea kumaliza ndaani ya nne bora Epl na kushinda kombe la Europa Conference Ligi baada ya kuwa na wakati mgumu Manchester akishindwa kutamba chini ya kocha Erik Ten Hag na badaye Ruben Amorim.

Kinachosubiriwa kuona iwapo atarejea katika kambi ya Manchester ama atasaka makao kwingineko msimu ujao.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version