Sports

Rais wa JKA Kenya Wakili George Kithi atangaza udhamini kamili kwa Wanakarate wa Kilifi

Published

on

Rais wa Japan Karate Association Kenya, wakili George ametangaza kuwa mdhamini mkuu wa timu za Karate kutoka Kilifi kushiriki katika Mashindano ya Desemba yajayo.

Mashindano ya Desemba yatatumika kama mashindano rasmi ya kuchagua timu ya taifa itakayoshiriki kwenye Kombe la Dunia la JKA,”Tumejitolea kuhakikisha kwamba kila kanda inapata nafasi ya kuonyesha wapiganaji wake bora, na kwamba hakuna kipaji kinachopuuzwa kwa sababu ya changamoto za kifedha. Kwa kudhamini timu hizi, tunalenga kusawazisha uwanja wa mashindano na kuhamasisha wakarateka wachanga kote nchini kujitahidi zaidi, kuwa na ndoto kubwa na kuamini katika uwezo wao,” amesema Wakili.

“Ninaziita dojo zote, wakufunzi na wakarateka wote kujiandaa kwa nidhamu na shauku. Haya si mashindano tu hii ni nafasi ya kuvaa rangi za taifa kwa fahari na kuonyesha ulimwengu nguvu, ustadi na roho ya Karate ya Kenya.”

“Tushirikiane wote huko Kilifi kuandika historia na kuweka viwango vipya vya ubora katika sanaa ya mapigano hayo.”

Mashindano hayo yatafanyika jijini Nairobi ugani Nyayo.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version