Sports
Nairobi United Ndio Mabingwa FKF Cup
Kilabu ya Nairobi United ndiyo mabingwa wa kombe la FKF Cup baada ya kunyuka Gor Mahia magoli 2-1 uwanjani Ulinzi Sports Complex hapo jana.
Kiungo Frank Ouya aliwatanguliza Nairobi United dakika ya 6 kabila ya Ben Stanley Omondi kuchomolea Kogalo dakika ya 37.
Goli la ushindi la Nairobi United lilitiwa kambani na Enock Machaka dakika ya 73 kipindi cha pili. United sasa ambao wanaingia FKF PL kwa mara ya kwanza itawakilisha Kenya kwenye taji la Mashirikisho Afrika CAF Confederation.
Katika mechi ya kusaka nafasi ya Tatu Muranga Seal 1-0 Mara Sugar.