News

Mwinyi: Serikali izuie Ubomozi wa Nyumba Elfu moja Changamwe

Published

on

Viongozi wa kisiasa kaunti ya Mombasa wanaitaka serikali kuingilia kati na kuzuia ubomozi wa nyumba zaidi ya elfu moja katika maeneo ya Chaani, Migadini, Lilongwe na Portreitz katika eneo bunge la Changamwe.

Wakiongozwa na Mbunge wa Changamwe Omar Mwinyi, viongozi hao wamesema baadhi ya wanasiasa walio uongozini wamekuwa wakisaidia mabwenyenye kunyakua ardhi za wananchi walalahoi.

Akizungumza na Wanahabari katika eneo bunge lake, Mwinyi ameitaka serikali kutafuta suluhu la kudumu la migogoro ya mashamba katika kaunti ya Mombasa na eneo la Pwani kwa jumla.

Mbunge huyo hata hivyo amewataka wanasiasa kukoma kuwanyanyasa wananchi na badala yake kuwahudumia bila ubaguzi ili kuzikabili changamoto mbalimbali mashinani.

Kauli yake imejiri baada ya familia nyingi katika maeneo ya Chaani, Migadini, Lilongwe na Portreitrz kulalamikia ubomozi wa nyumba zao bila mikakati mwafaka ya kuhamishiwa katika ardhi mbadala.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version