News

Mwinyi, awaonya wakenya dhidi ya siasa za migawanyiko

Published

on

Baadhi ya viongozi katika kaunti ya Mombasa wakiongozwa na mbunge wa Changamwe Omar Mwinyi wamewakosa wananchi pamoja na viongozi dhidi ya kuendeleza siasa za migawanyiko, taifa linapojiandaa kwa kipute cha uchaguzi mkuu ujao wa mwaka wa 2027.

Mwinyi alisema taifa la Kenya linahitaji maendeleo na sio siasa zinazosababisha migawanyiko kwa Wakenya kwa misingi ya vyama vya kisiasa na ukabila.

Mwinyi pia aliwakosa wale ambao wanawadhalilisha wanawake kutokana na misimamo yao ya kisiasa.

“Huyu Zamzam anaheshimiwa kitaifa, wewe mtu wa Mombasa kwa nini umtukane. Kwa hivyo wenye siasa hizo wakome’’Alisema Mwinyi.

Naye Gavana wa kaunti ya Mombasa Abdulswamad Shariff Nassir aliwahimiza viongozi kutoka mirengo mbalimbali ya kisisa kushirikiana ili kuwe na amani katika taifa hili la Kenya kauli ambazo zimeungwa mkono na baadhi ya wawakilishi wa wadi katika kaunti hiyo.

“Mimi nawaomba tuungane kama viongozi na tuweka tofauti zetu za kisiasa kando, 2027 ikifika mwenyezi Mungu atatujalia yule ambaye atakuwa gavana maana uongozi unatoka kwa Mungu, binadamu ni sababu’’, alisema Nassir.

Taarifa ya Janet Mumbi

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version