News

Mwadime, Amewataka Vijana Kujisajili na Vyuo vya Kiufundi

Published

on

Katibu katika Wizara ya Leba nchini Shadrack Mwadime amewataka vijana ambao wana ujuzi mbalimbali lakini hawana stakabadhi kujisajili na Mamlaka ya kitaifa ya mafunzo ya viwanda NITA ili waweze kupata vyeti na ajira. 

Kulingana na Mwadime, Mamlaka ya NITA imekuwa mstari wa mbele katika kutoa vyeti ambavyo wakenya wanaweza kupata ajira katika mataifa ya ughaibuni na zenye malipo bora.

Akizungumza wakati wa kutoa vyeti hivyo kwa wanafunzi wa chuo cha kiufundi cha Dzitsoni katika kaunti ya Kilifi, Mwadime amesema tayari kuna wanafunzi zaidi ya elfu 20 ambao wamesajiliwa kufanya mitihani katika Mamlaka hiyo ili waweze kupata vyeti hivyo. 

Kwa upande wake Mwenyekiti wa wa kamati ya Leba katika bunge la kitaifa ambaye pia ni mbunge wa Kilifi Kusini Ken Chonga, amewahimiza vijana kujiunga na vyuo vya kiufundi huku Mwenyekiti wa bodi ya Mamlaka ya NITA Aden Noor Ali akisema kila mwaka wanahamasisha wanafunzi zaidi ya laki moja kujisajili na NITA.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version