News

Liverpool Kutangazwa Bingwa Mpya Epl

Published

on

Miamba wa Uingereza kilabu ya Liverpool kutangazwa mabingwa wapya wa ligi kuu EPL Wikendi hii iwapo watatoka sare ya aina yoyote dhidi ya kilabu ya Tottenham Hotspurs ugani Anfield.

Haya yanajiri baada ya kilabu nambari mbili Arsenal kudondosha alama mbili muhimu siku ya jumatano dhidi ya Crystal Place timu hizo zikiisha sare ya magoli 2-2 uwanjani Emirates na kudidimiza matumaini yake ya kutwaa ubingwa wa Epl msimu huu.

Beki Jacob Kiwior aliweka uongozini The Gunners kunako dakika 3 kabla ya Palace kusawazisha kupitia kwa kiungo mshmabulizi Eze Oberechi kunako dakika ya 22 na licha ya kuchukua uongozi mwingine kupitia Leandro Trossard dakika ya 46,kilabu ya Palace ilijibu dakika ya 84 kupitia kwa mshambulizi Jean Philip Mateta.

Matokeo haya yanawacha Liverpool nafasi ya kwanza na alama 79 nayo Arsenal nafasi ya pili na alama 67 nayo mancity wakiwa nafasi ya tatu na alama 61 nayo Nottingham Forest ni ya nne na alama 60 mkiani ni vilabu vya Ipwisch Town,Leicester city na Southampton mtawalia.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Trending

Exit mobile version